• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

WANANCHI KATA YA NAMUPA WATAKIWA KUZINGATIA VIGEZO KUHUSU KAYA MASIKINI

Posted on: November 13th, 2021

Wananchi wa Kijiji cha Namupa na Muungano Kata ya Namupa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama Mkoani Lindi wametakiwa kuzingatia vigezo na kanuni zilizotumika wakati wa kuzitambua kaya masikini kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya masikini (TASAF).

Rai hilo limetolewa tarehe 12/11/2021 na Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mtama Bi. Sharifa Tapalu alipokuwa akitoa majibu ya maswali yaliyoulizwa na wananchi wa Vijiji hivyo walipohoji kwanini wazee wameachwa na kuchukuliwa vijana wenye nguvu za kufanya kazi zao na kuwa walengwa kwenye mpango huo.

Kabla ya kutoa ufafanuzi wa swali hilo Bi. Sharifa alianza kueleza dhumuni la Mradi wa TASAF ambapo amesema lengo kuu ni kunusuru kaya masikini na kuleta mabadiliko chanya katika jamii. Alisema kuwa watu wengi wanaamini kuwa TASAF ni kwa ajili ya wazee na kuwataka wafahamu vigezo vinavyotumika wakati wa utambuzi wa kaya hizo.Aliongezea kusema kuwa kaya wanazozilalamikia zilitambuliwa na wananchi wenyewe kupitia mikutano ya hadhara ikiwa ni hatua za awali za zoezi la kuibua mradi huo.

Alivitaja vigezo hivyo ikiwa ni pamoja na:

  1. Kaya inayoshindwa kupata milo 3 kwa siku
  2. Hali ya upatikanaji wa huduma za Afya
  3. Hali ya upatikanaji wa huduma za elimu.
  4. Kaya yenye watu walemav
  5. Kaya yenye makazi duni.

Mkutano huo uliongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtama Ndg. Mahmoud Kimbokota katika kijiji cha Namupa kwa lengo la kuhamasisha wananchi wa vijiji hivyo kuendelea kujitolea kufukia mitaro ya maji mradi wa Namupa-Mahiwa unaofadhiriwa na Kanisa la Anglikana pamoja na  kusikiliza kero za wananchi.

Awali ya hapo, mjadiliano  mzito uliendelea mkutanoni hapo kujadili suala la Wananchi hao kuonekana kutokubali kuendelea kujitolea kwenye mradi huo ambapo walipata nafasi ya kutoa sababu zao ikiwa ni pamoja na kukosa ushirikishwaji wa viingozi kwenye utekelezaji, wataalamu kuzuia kufukia ili kupisha uwekaji wa vituo vya kupumzikia maji, uchache wa vilula vya maji. 

Mwanchi akitoa hoja

Afisa Utumishi akiongoza mjadala

Kufuatia majadiliano hayo, Kaimu Mkurugenzi ambaye ni Afisa Utumishi Halmashauri ya Wilaya ya Mtama Mahmoud Kimbokota aliwataka wananchi hao kuweka pembeni tofauti zao na waendelee kujitolea na kwamba wananchi hao walikubaliana kuendelea na shughuli ya ufukiaji wa bomba la maji. Aidha , Kimbokota aliwaelekeza watumishi na wataalamu mbalimbali kufanya kazi kwa uadilifu, uaminifu na uzalendo wa hali ya juu ili kutoa huduma bora katika jamii.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.