Kamati ya lishe Halmashauri ya Wilaya ya Mtama leo tarehe 4 juni 2025 imefanya kikao maalum cha tathmini ya utekelezaji wa afua za lishe kwa ngazi ya Halmashauri kilicholenga kupima hatua zilizofikiwa katika kuboresha hali ya lishe kwa Wananchi, kikao hiko kimefanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Halmashauri ya Mtama.
Akizungumza wakati wa kikao hiko Bi: Emma Lunojo Mwenyekiti wa kamati ya lishe kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Mtama amewataka wajumbe wa kamati hiyo kuhakikisha wanatoa elimu na hamasa ya kutosha kwa jamii juu ya umuhimu wa kutekeleza afua za lishe ikiwemo ufuatiliaji wa afya kwa watoto na akina mama wajawazito.
“Niwajibu wetu kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi kuhusu lishe ili kila mwananchi awezekuchukua hatua stahiki, Tukiwa kama viongozi na wataalamu katika maeneo yetu tunapaswa kuwa mstari wa mbele katika kutoa hamasa na elimu endelevu kuhusu lishe bora” alisema Bi: Emma Lunojo.
Aidha katika kikao hiko idara mbalimbali ziliwasilisha taarifa zao za utekelezaji wa afua za lishe zikiwemo idara ya Afya, Elimu Msingi, Elimu sekondari, kilimo na mifugo pamoja na idara ya Maendeleo ya Jamii, Taarifa hizo zilionyesha hatua mbalimbali zilizochukuliwa na changamoto zilizojitokeza katika kutekeleza shughuli za lishe katika idara husika.
Hatahivyo, Ndugu Gozbert Henerico Mratibu wa lishe Halmashauri ya Mtama alisisitiza kuwa kikao hiko ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa lishe kitaifa na kinaweka msingi imara wa ushirikiano baina ya sekta mbalimbali katika kuimarisha hali ya lishe ndani ya Halmashauri ya Mtama.
Box 328 Lindi
Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc
Simu ya mezani: 0222061
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@lindidc.go.tz
Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.