• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

WANAFUNZI 564 WAPATIWA TAULO ZA KIKE MTAMA DC.

Posted on: July 29th, 2021

Wanafunzi hao wamenufaika kupitia Programu iliyoanzishwa Mwezi Julai chini ya uratibu wa Mama Rhobi Nnauye mke wa Mbunge wa Jimbo la Mtama kwa niaba ya Mh. Nape Moses Nnauye Mbunge wa jimbo hilo kwa lengo la kupunguza changamoto zinazowakabili wanafunzi wa kike na kuongeza Ari na kujiamini katika kipindi kizima cha maandalizi ya mitihani yao ya kidato cha nne.


Mama Rhobi Nnauye amekamilisha zoezi la ugawaji wa taulo za kike tarehe 29 Julai 2021 katika shule za sekondari kata ya Nyangamara na Mandwanga ndani ya Halmashauri hiyo akiambatana na wenyeji wake Diwani viti Maalumu kata ya Nyangamara Mh Asha Nguli, Mwenyekiti wa UWT  kata ya Nyangamara Bi. Zainabu Madevu na Makamu mwenyekiti Bodi ya kituo cha Afya Nyangamara na kufanikiwa kutoa jumla ya taulo 118 kwa wanafunzi zaidi ya 64 katika shule ya sekondari Nahukahuka, Mandwanga, Chiuta, Mbawe na Litipu kwa wanafunzi wa kike kwa kidato cha nne.


Katika zoezi hilo Mama Rhobi Nnauye alipata nafasi ya kuzungumza na wakuu wa shule na baadhi ya walimu walezi ili kubaini changamoto za kiutendaji ambapo wengi wao wamezungumza kuhusiana na suala la muhamko mdogo wa wazazi juu ya elimu kwa watoto wao jambo ambalo linapelekea kurudisha nyuma jitihada za walimu na wanafunzi hao kufanya vizuri katika masomo yao pia wametoa shukurani zao kwa msaada wa taulo hizo kwanini zitapunguza ongezeko la utoro shuleni. Aidha Mama Rhobi Nnauye alipata nafasi ya kuzungumza na wanafunzi wa kike wa kidato cha nne ambapo amewataka wanafunzi hao kutochanganya mapenzi na masomo pia amesisitiza zaidi ushirikiano baina yao na kusaidiana katika masomo ili kufikia malengo yao. " Najua kila mtu ana malengo yake lakini hatuwezi kufikia malengo Hayo bila ushirikiano, niwasihi sana msichanganye mambo yasiyohusiana na masomo mnachotakiwa ni kupambania ndoto zenu na kila kitu kinawezekana." Rhobi Nnauye.

Kwa upande wa diwani viti maalumu kata ya Nyangamara ametoa shukurani kwa Mama Rhobi kwa kuoneshwa kuwajali watoto wa kike lakini pia amewahasa wanafunzi kuyasikiliza yaliyozungumzwa na mgeni rasmi huku akitoa msisitizo zaidi kuhusu kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yao.

Zoezi lilianza Julai 2021 na Mpaka sasa amefanikiwa kugawa taulo za kike zaidi ya 1,300 kwa wanafunzi wa kike wa kidato cha nne 564, kwenye sekondari 17 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama huku akiwa na matarajio ya kugawa taulo za kike 3,000 ndani ya Halmashauri hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.