• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA YAKABIDHI MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI.

Posted on: November 16th, 2021

Halmashauri ya Wilaya Mtama imetoa mikopo yenye thamani ya Tshs. 59,600,000/= kwa vikundi 21 vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu. Mikopo hiyo imetolewa tarehe 15 Novemba 2021 na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe.  Shaibu Ndemanga katika viwanja vya Halmashauri hiyo.

Akikabidhi pikipiki na fedha kwa vikundi hivyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi Zainab Telack, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga aliwataka wajasirimali walikopa kuhakikisha kwamba wanafanyia kazi zilizokusudiwa ili kujiinua kimapato na kurejesha fedha hizo ili zitumike kuwakopesha wengine.

Vilevile aliwataka vijana wa bodaboda kutumia pikipiki hizo kujiinua kiuchumi na si katika anasa na kuwarubuni wanafunzi hali ambayo Serikali haitawafumbia macho katika suala hilo. 

 "Tumewapa mikopo kuchukua abiria, hao wanafunzi ni abiria  acheni kutumia pikipiki kama chambo kwa watoto wa shule. Tunawatakeni muwaache watoto wa shule wasome na watimize ndoto zao" alisema Ndemanga na kuongeza kuwa wakibaini wanatumia pikipiki hizo katika uhalifu wa aina mbalimbali ukiwemo kurubuni watoto wa kike watawapokonya.

Kutokana na kuwepo kwa changamoto za ongezeko la mimba za utotoni zinazosababishwa na madereva wa bodaboda Mhe. Ndemanga amesema kuwa wao wataendelea kuwaangalia kwa jicho kali kuona kwamba hawatumii rasmimali hizo kuwakwamisha wanafunzi.

Akisoma taarifa fupi ya mikopo hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, George Mbilinyi alisema vikundi  8 vya vijana vimekopeshwa pikipiki, vikundi 10 vya wanawake na vikundi 3 vya wenye ulemavu vilikopeshwa fedha.

Aidha Mbilinyi alieleza kuwa katika kipindi cha Robo ya Kwanza Mwaka 2021/2022 Halmashauri ya Wilaya Mtama imetoa Mikopo yenye thamani ya Tshs. 59,600,000/= kwa  vikundi 21 vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu. Aliongezea kwamba Mikopo hiyo imetolewa kwa mujibu wa sheria inayogusa mikopo ya Halmashauri inayotokana na makusanyo ya ndani ambapo Halmashauri zinapaswa kutenga asilimia 10% ya mapato yake ya ndani yanayotokana na vyanzo vyake kwa ajili ya kukopesha vikundi vya Wajasiriamali vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu.  

Mkurugenzi akisoma taarifa fupi ya mikopo.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Karim Ali alisema kwamba vijana wameshukuru kwa kukopeshwa pikipiki kwani itawasaidia kuinua uchumi wao na kwamba watarejesha mkopo huo kwa muda muafaka waliolekezwa.

Vikundi vya pikipiki vilivyopata mkopo huo ni vikundi vya vijana wa kikundi cha Tumeungana Bodaboda kutoka Kata ya Majengo Pikipiki 4, Kikundi cha UWAMI kutoka Mtama Pikipiki 4, na Kikundi cha Vijana na Maendeleo Namupa Pikipiki 3.  Pikipiki hizo 11 zina  thamani ya Tshs. 27,500,000/=  lakini pia vikundi vya wanawake 10 vilipokea kiasi cha Tshs. 27,100,000/= pamoja na vikundi 3 vya walemavu vilipata Tshs. 5,000,000/= na kwamba  Vikundi hivyo  3 vinawakilisha vikundi vingine 21.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.