• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

"TUTUMIE MIKOPO YETU KWENYE MALENGO TULIYOKOPEA". NAIBU WAZIRI VIWANDA NA BIASHARA."

Posted on: September 28th, 2021

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Exaud Kigahe akiwa kwenye ziara yake ya kikazi Wilayani Lindi tarehe 28 Agosti 2021 katika ukumbi wa Mikutano wa Mkoa alipokuwa akizungumza na Maafisa Kilimo na ushirika, Wadau mbalimbali wa kilimo, wawakilishi wa Vyama vya Msingi pamoja na wakulimwa wa zao la Korosho.  Lengo la ziara hiyo ni kujifunza namna Mfumo wa Stakabadhi Ghalani unavofanya kazi, faida pamoja na kusikiliza changamoto zitokanazo na Mfumo huo ili kuzipatia ufumbuzi yakinifu.  Aidha alipata nafasi ya kusikiliza michango mbalimbali kutoka kwa wajumbe wa kikao hicho.

Miongoni mwa wajumbe hao ni pamoja na Werner Chiwembi mkulima wa zao la Korosho Halmashauri ya Wilaya ya Mtama aliyeeleza kuwa licha ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali lakini kuna  faida nyingi  za Mfumo wa Stakabadhi Ghalani ikiwa ni pamoja na uhakika na usalama wa upatikanaji na utunzaji wa fedha mara baada kuuza mazao huku akiongeza kuwa Mfumo huo umekuwa chachu ya mafanikio ya wakulima wengi kwani unasaidia katika harakati za kusomesha watoto pamoja na kutunza familia na Taifa kwa ujumla.  Ametoa ushauri kwa viongozi kuwa Mfumo huo hauna budi  kuendelea ikiwezekana hata kwa aina nyingine ya mazao kama vile mbaazi na mahindi.

Kwa upande wa mwakilishi wa NBC Lindi Ndg. George Malibiche alieleza manufaa yanayopatikana kupitia Mfumo huo ikiwa ni pamoja na ongezeko kubwa la idadi ya wakulima wanaofungua akaunti mpya kwenye benki hiyo, kutanua wigo wa utoaji wa huduma katika maeneo mbalimbali kwa kutumia mawakala lakini pia Mfumo umepelekea Benki hiyo kubuni mbinu mpya za bidhaa na huduma kama vile mikopo kwa wakulima, bima za wakulima pamoja na mpango wa kuanzishwa kwa akaunti maalumu za wakulima.

Naye Diwani Viti Maalumu Tarafa ya Mtama Mh. Mariamu Kharifa amemuomba Naibu Waziri kuwekeza zaidi kwenye viwanda kwani ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mtama kuna maeneo  pamoja na malighafi ya kutosha kwa uendeshaji wa shughuli za viwanda ikiwemo zao la Korosho pamoja na Miwa na  kwa kufanya hivyo kutapelekea maendeleo ya mtu mmojammoja na Taifa kwa ujumla.

Akitolea ufafanuzi wa michango mbalimbali iliyowasilishwa na wajumbe wa kikao hicho, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mh. George Kigahe amesema kuwa atahakikisha anatoa hamasa katika uwekezaji wa ndani ili kuinua na kuikuza sekta ya viwanda na biashara. Vilevile ametoa maelekezo kwa viongozi wa vyama vya msingi  kuhakikisha wakulima wanapata stahiki zao mapema iwezekanavyo ili kudhibiti uuzaji holela wa mazao huku akisisitiza zaidi kuhusiana na suala la uadilifu kuanzia ngazi ya wakulima hadi viongozi wa Ushirika pamoja na Vyama vya Msingi kwa kuzingatia ubora na usafi wa mazao pindi yanapofikishwa ghalani kwa hatua ya uuzaji na kwamba kwa  kufanya hivyo kutapelekea ushindani mzuri wa soko la kitaifa na kimataifa. Sambamba na hilo, Mh. Kigahe amewataka wakulima kuhakikisha wanakuwa na hati za mashamba yao ili kurahisisha zoezi la upatikanaji wa Mikopo lakini pia ni lazima wahakikishe wanalipa madeni ya mikopo hiyo kwenye Mabenki husika. “ naomba nisisitize hili ndugu zangu wa Lindi tusikwepe kulipa madeni lakini tuitumie kwa usahihi sio Umekopa kwa ajili ya kupulizia mikorosho lakini wewe unakwenda kupulizia nyumba ndogo; TUTUMIE MIKOPO YETU KWENYE MALENGO TULIYOKOPEA”

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.