• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

TASAF YATOA MAFUNZO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA

Posted on: August 30th, 2021

Wawezeshaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kutoka ngazi ya Taifa, Agosti 30, 2021 wametoa Mafunzo ya kutoa huduma za kitaalamu kwa jamii katika utekelezaji wa Miradi ya kutoa Ajira za Muda  kwa Walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini kupitia wasimamizi wa Miradi kutoka Vijiji 69 vya Halmashauri ya Wilaya ya Mtama kwa lengo la kujenga uelewa katika utekelezaji wa Miradi hiyo.  Mafunzo hayo yalifunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama Mh. George Mbilinyi katika Ukumbi wa Mikutano.

Akifungua mafunzo hayo yaliyoambatana na  Usomaji wa hotuba  kwa washiriki wa mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama Mh. George Mbilinyi amesisitiza zaidi kuhusu uaminifu na uadilifu katika utekelezaji wa Miradi hiyo “Napenda kuwasisitiza kuwa waadilifu tunapoenda kuanza utekelezaji wa miradi hii, tukafanye kazi kwa uaminifu na uadilifu wa hali ya juu ili tufikie malengo ya serikali kupitia kipini cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF ya kupunguza umasikini na kuchochea ukuaji wa uchumi . Ni imani yangu kwamba mtasimamia miradi hii kwa ubora unaotakiwa na kwa kuzingatia miongozo na maelekezo mtakayopewa katika mafunzo haya. Sitarajii kusikia kwa msimamizi yeyote katika eneo lake la kazi kunakuwa na mradi uliofanywa chini ya kiwango au mradi usiofanana na thamani ya fedha, mimi mwenyewe kupitia maafisa wangu tutakuja kuwakagua ili tutumie vizuri rasilimali fedha na kufiki malengo yetu, hivyo hatua kali zitchukuliwa kwa msimamizi yeyote atakayefanya kinyume na maelekezo mtakayopatiwa”. Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri.

Sambamba na hilo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri alichukua fursa hiyo  kuwakumbusha washiriki wa Mafunzo hayo kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa UVIKO19 kwa kufuata hatua mbalimbali za kujikinga dhidi ya ugonjwa huo pindi watakapokuwa katika maeneo yao ya utekelezaji wa Miradi hiyo.

Kwa upande wake Afisa ufuatiliaji  wa TASAF ambae pia ni mwezeshaji kitaifa wa mafunzo hayo Ndg. Tumain Michael Yanai, ameelezea maana ya dhana ya  Miradi ya Ajira za Muda kwamba ni kazi zinazofanywa na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini kwa muda husika na kulipwa ujira,  huku akitoa malengo ya Miradi hiyo ikiwa ni pamoja na kuziwezesha kaya masikini kujipatia kipato, kupata miundombinu itakayonufaisha Walengwa na jamii kwa ujumla pamoja na kuongeza ujuzi wa utendaji wa shughuli mbalimbali katika jamii.

Naye mwezeshaji wa Mafunzo Kitaifa wa Miradi ya Ajira za Muda , ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya jamii Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Ndg. Sky Thomas amewasa washiriki kutojihusisha na Rushwa wakati wa usimamizi wa miradi hiyo “Tukafanye kazi kwa moyo wa kujitolea kwani tunatamani Miradi ya awamu hii iwe yenyekufanana na thamani ya fedha,  ubora, pamoja na kiwango kinachotakiwa. Tusiwe watu wa kupokea rushwa katika ukaguzi wa utekelezaji na hatutegemei katika Wilaya ya Mtama kuwepo kwa udanganyifu kwani hupelekea Miradi mbalimbali kutekelezwa chini ya kiwango, hivyo basi ni muhimu kujiridhisha kwamba Mlengwa wako amekamilisha kazi ya siku husika”. Alisema  Sky Thomas.

Mafunzo hayo yanayotarajiwa kumalizika Septemba 2, 2021 yatakua ni chachu ya Mafanikio kwa Walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini, lakini pia ni  urahisishaji wa utekelezaji kupitia  wawezeshaji wa  Miradi ya kutoa Ajira za Muda zitakazodumu kwa  muda wa Miezi 6 .



Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.