• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

NG'OMBE ZAIDI YA 9,000 WILAYANI LINDI KUOGESHWA KWENYE MAJOSHO NA KUPATIWA CHANJO YA MAGONJWA.

Posted on: December 18th, 2019

Jumla ya Ng'ombe 9774 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Lindi (Mtama) Mkoani Lindi wanatarajia kupitishwa na Kuogeshwa katika majosho mbali mbali ya Wilaya hiyo kwa lengo la kupatiwa chanjo dhidi ya Magonjwa yaenezwayo na kupe (Ndigana kali).

Hayo yameelezwa na Daktari wa mifugo wa Halmashauri hiyo Dokta Joseph Sijapenda wakati wa uzinduzi wa zoezi la kuogesha Ng'ombe katika Josho la Gereza la kingurungundwa lililopo kata ya kitomanga Wilayani humo.

Katika uzinduzi huo jumla ya Ng'ombe 400 kutoka kata ya kitomanga na maeneo jirani ya wilaya hiyo walipatiwa chanjo dhidi ya Magonjwa yaenezwayo na kupe.

Akizungumza katika uzinduzi huo Sijapenda lisema kuwa Halmashauri yao imepokea jumla ya lita 54 za dawa kwa ajili ya kuwapatia Ng'ombe 9774 waliopo katika Wilaya hiyo ambapo lita 42 ni dawa aina ya mitraz na lita 12 aina ya palanents Huku akifafanua kuwa lengo kubwa la Serikali kuanzisha zoezi hilo ni kuhamasisha wafugaji kuogesha Mifugo yao ili kuwa na ufugaji wenye tija.

Hata hivyo Sijapenda aliongeza kuwa baada ya uzinduzi huo wafungaji watalazimika kuwapeleka Ng'ombe wao kila siku za juma mosi katika majosho yaliyo karibu nao kwa ajili ya kuogeshwa na kupatiwa kinga hiyo.

Nae mwakilishi wa Wizara ya Mifugo na uvuvi kutoka kituo cha huduma na mifugo kanda ya kusini jostinian lutatina alisema kuwa Magonjwa ya yaenezwayo na kupe hususani Ndigana kali ni miongoni mwa changamoto kubwa katika maendeleo ya sekta ya Mifugo kwa kuwa yanasababisha vifo vingi vya mifugo hapa Nchini.

"hapo mwanzo uogeshwaji wa mifugo ulikuwa unagharamiwa na Serikali ambapo wafugaji walikuwa wanaogeshwa bure, lakini kutokana na ufinyu wa bajeti na mabadiliko ya Sera gharama za uogeshwaji zilibaki kwa wafugaji wenyewe na matokeo yake wafugaji wengi walikosa mwamko wa kuogesha mifugo yao" alisema.

Hata hiyo lutatina alisema kuwa Viuwatilifu hivyo vilivyotolewa na Serikali vitatumika kama ruzuku ambapo wafugaji watalazimika kulipa shilingi mia sita 600 kwa ng'ombe mmoja kila anapokwenda kumpatia chanjo hiyo kwa kipindi cha miezi sita ili kiasi kitakachopatikana kiweze kununua dawa zingine.

Nae Mwenyekiti wa wafugaji kata ya kitomanga Ntima Ngusa aliishukuru Serikali kwa kuwapatia ruzuku hiyo ya viuwatilifu kwani itapunguza gharama ya uendeshaji katika kuhudumia mifugo yao.

Ngusa alisema kuwa hapo awali walikuwa wanalazimika kutumia zaidi ya shilingi elfu mbili kwa ajili ya kununua dawa ya kuogesha Ng'ombe mmoja kwa siku.

Nae mkuu wa Wilaya ya Lindi ambae ndie aliekuwa Mgeni rasm katika uzinduzi huo aliwataka wafugaji kujitokeza kwa wingi siku zitakazopangwa kwa ajili ya kuwapatia chanjo mifugo yao Ili waweze kunusuru mifugo yao na magonjwa.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.