• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

"MTAMA NI MAKAO MAKUU YA JIMBO NA HALMASHAURI LAZIMA TUIPE HESHIMA". Mh. NAPE MOSES NNAUYE.

Posted on: July 28th, 2021

Hayo yamesemwa leo Julai 28 2021 na Mbunge wa Jimbo la Mtama Mh. Nape Moses Nnauye katika Uwanja wa Mkorosholofa kijiji cha Mihogoni wakati akitolea ufafanuzi wa hoja na maswali yaliyoibuka kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Mvuleni na Mihogoni katika mkutano wa adhara na wananchi hao.

Katika ziara yake hiyo wananchi walipata nafasi ya kuuliza maswali na kutoa mapendekezo yao kuhusu mambo mbalimbali ya kimaendeleo ambapo miongoni mwa hoja na maswali yaliyoibuka na kupatiwa ufafanuzi kutoka kwa Mh. Mbunge ni pamoja na suala la umeme, maji, pamoja na upimaji wa mji.

Akitolea ufafanuzi wa hoja na maswali mbalimbali yaliyoibuka katika ziara yake, Mh Nape ametoa ahadi kuhusu suala la umeme kuwa atalifanyia kazi. "Niwaahidi Kuwa lazima tuongeze nguvu kwenye suala ya umeme ndani ya Jimbo na niwahakikishie tutamaliza tatizo la umeme. Mtama ndio makao  makuu ya Jimbo na na Halmashauri hivyo ni lazima tuipe heshima". Alisema Mh Nape Mbunge Jimbo la Mtama katika kijiji cha Mihogoni. Aidha ameendelea kusisitiza kuhusu bei ya umeme ambayo ni 27000Tsh na kwamba nguzo za umeme zitapatikana bure bila Malipo. Sambamba na hilo Mh Nape amesema zaidi ya shilingi bil.5 zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu na miradi ya maji.

Aidha Mh. Nape ametolea ufafanuzi kuhusu ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Mtama ambapo amesema kuwa kituo cha afya kitajengwa katika kijiji cha Mpenda kata ya Mtama. Vilevile amesema serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule za sekondari zipatazo sita na moja itajengwa Mtama ikiwa ni shule ya kisasa yenye mabweni kwa lengo la kuinua sekta ya elimu.

Kuhusu suala la upimaji wa mji, amesema kuwa ni zoezi linalohitaji kiasi kikubwa cha fedha hivyo basi kupitia kwa waziri wa ardhi wameomba fedha ili kurahisisha zoezi hilo. Sambamba na hilo amewaomba wananchi kukabiliana na changamoto ya ubomoaji wa baadhi ya majengo na mimea wakati wa zoezi la upimaji wa mji likiendelea.

Mh. Nape amewaomba wananchi wa kata ya Mtama kuweke tofauti za kisiasa Mandi na badala yake kutoa ushirikiano na diwani wa kata ili kupelekea maendeleo, vilevile amemtaka diwani wa kata ya Mtama kuzunguka katika maeneo yake ya kata ili kufahamu changamoto zinazowakabili wananchi wake. Pia ametoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kufanya katika miradi mbalimbali ya kimaendeleo ili kujipatia kipato.

Mh. Nape anaendelea na ziara yake ya kikazi katika Jimbo hilo ndani ya Halmashauri ya Mtama ambapo Leo amepata nafasi ya kuzunguka katika vijiji vya Mpenda, Mihogoni, na Makonde kata ya Mtama na kuzungumza na wananchi kuhusu mambo mbalimbali ya maendeleo jimboni hapo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.