• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

MTAMA DC YAMUENZI BABA WA TAIFA KWA KUZUNGUMZA NA WAZEE WA MTAMA.

Posted on: October 15th, 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama Ndg. George Emmanuel Mbilinyi jana Oktoba 14 2021 ameongoza kikao cha mazungumzo na baadhi ya wawakilishi wa wazee wa Mtama ikiwa ni ishara ya  kumuenzi aliyekuwa Rais wa awamu ya kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mwl. Julis Kambarage Nyerere lakini pia kujitambulisha rasmi kwa wazee hao. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya Mh. Othmani Hongonyoko, wakuu wa Idara mbalimbali, Madiwani pamoja na watendaji wa Kata na Vijiji vya Mtama na Majengo.

Ndugu Mbilinyi amewaomba wazee hao kutoa ushirikiano wa kiutendaji ili kufikia lengo la kuleta maendeleo kwa wananchi huku akiwahimiza kuwahamasisha vijana wao kujitolea kwenye Miradi mbalimbali ya kimkakati. Pamoja na hilo, Mkurugenzi huyo amewaomba wazee hao kuondoa tofauti za kiitikadi za Siasa na badala yake wajikite zaidi katika kidumisha na kuendeleza amani, upendo na mshikamano ndani ya Halmashauri na Taifa kwa ujumla.

Wazee hao pia walipata nafasi ya kutoa hoja zao ambapo kwa ujumla wametoa pongezi kwa Mkurugenzi huyo kwa kuwapa thamani kubwa ya kuwaita na kuzungumza nao lakini hawakusita kutoa changamoto na kero zao ikiwa ni pamoja na uchache wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya . Sambamba na hilo wameahidi kutoa ushirikiano katika ujenzi wa Mtama mpya kwani ni matamanio yao ya muda mrefu kuona maendeleo ndani ya Halmashauri hiyo.

Akitolea ufafanuzi wa tatizo la uchache wa dawa, Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Dismas Masulubu amesema kuwa  kukamilika kwa  Mradi wa ujenzi wa  kituo cha afya cha Mtama kutarahisisha upatikanaji wa dawa zitakazotibu magonjwa ya wazee  kwani dawa hizo  zinatolewa kulingana na ngazi ya kituo cha huduma na ukubwa wa tatizo. Aidha amewathibitishia kuwa  Bohari Kuu ya Madawa (MSD) tayari imesambaza dawa kwa asilimia 82% hivyo basi changamoto hiyo imetatuliwa.

Mkurugenzi akiwa kwenye kikao na wananchi wa Pangatena

Awali ya hapo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama alikutana wa wananchi wa Hingawali, Njonjo na Pangatena kwenye Mkutano uliofanyika Kata ya Pangatena uliolenga kusikiliza changamoto pamoja na kuondoa migogoro na migongano baina ya wananchi wa Kata hiyo. Ametoa maelekezo kwa watendaji wa  Vijiji na Kata kutatua matatizo yanayojitokeza kwenye maeneo yao ya kazi na sio kusubiri mikutano ya viongozi wa ngazi za juu itakapofanyika. "Njia nzuri ya kutatua migogoro ni kuanza kushughulika nayo kwenye ngazi za chini". George Mbilinyi. Vilevile amewaelekeza watendaji hao kuwatumia wazee wa vijiji pindi wanapohitaji kupunguza migogoro mbalimbali.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.