• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

MKURUGENZI MTAMA DC AKUTANA WENYEVITI WA VIJIJI

Posted on: November 2nd, 2021


Ikiwa ni katika muendelezo wa vikao kazi mbalimbali , Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama Ndg. George Emmanuel Mbilinyi  Jana tarehe 1 Novemba 2021 amekutana na kuzungumza na Wenyeviti wa Vijiji vyote vya Halmashauri, katika kikao kazi hicho alihudhuria pia Mhe, Athumani Hongonyoko –Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Lindi pamoja na baadhi ya wataalamu wa Idara na vitengo mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mtama.

Dhima kuu ya kikao hicho ni kujitambulisha pamoja na kutoa taarifa ya mapokezi ya Miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania Mh. Mama Samia Suluhu Hassan ambayo ni pamoja na ujenzi wa Kituo cha Afya Tarafa ya Mtama, Fedha za miradi ya Maji, pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo kwa shule za Msingi na Sekondari lakini pia kugawa vyeti vya Hati  ya usajili wa Vijiji kwa Wwnyeviti hao.

Kwenye maelekezo ya namna ya usimamizi wa Miradi hiyo, Mkurugenzi  amewataka Wenyeviti hao kusimamia kwa  uzalendo na uaminifu mkubwa kwani miradi hiyo inakwenda kuwanufaisha wananchi wote katika maeneo mbalimbali, pia amewahimiza kutumia rasilimali zilizopo kama vile mawe, mchanga, kokoto na rasilimali watu ili kupunguza gharama za ujenzi  kwenye miradi hiyo.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji (W) aliwasisitizia Wenyeviti hao kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa kasi na kuhakikisha  inakamilika  kwa wakati huku wakizingatia viwango na ubora unaoendana na fedha zilizotolewa na kuongeza kuwa ni lazima wakafanye kazi kwa ushirikiano wa hali ya juu na watendaji wa vijiji, kata pamoja na kamati za ujenzi kwa kushauriana, kukosoana na kurekebishana kwa pamoja ili kufikia malengo na kuiendeleza Halmashauri na Taifa kwa ujumla.

Sambamba na maelekezo hayo, Mkurugenzi Mtendaji (W) alipata nafasi ya kutoa rai kwa Wenyeviti hao kutoruhusu wahamiaji pamoja na wafugaji kuingia kwenye vijiji vyao kiholela  na badala yake watumie taratibu na sheria ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima kati ya wafugaji na wakulima “maeneo mengi sana Tanzania hii  tunapata shida kusuluhisha migogoro ya wakulima na wafugaji,  musikubali kupokea hongo na kuruhusu wafugaji waingie kwenye maeneo yenu na kwamba kwa kufanya hivyo mutasababisha  matatizo makubwa katika jamii  kwani sisi tumezoea kuishi kwa amani na wakulima wetu. Kama wanahitaji maeneo lazima wafuate taratibu na pindi zitakapokamilika matangazo yatatolewa lakini kwa sasa hatuna maeneo kwa ajili ya wafugaji”  George Mbilinyi Mkurugenzi Mtama.

Mwisho kabisa alizungumzia suala la mapato na kuwataka wajumbe wa kikao hicho kuwa viongozi na  mabalozi wazuri kwa kuhakikisha mashine za kukusanyia mapato (POSS) zinafanya kazi kikamilifu na wasiruhusu watu kukwepa kulipa ushuru ili kuinua mapato ambayo yatakuwa chachu ya maendeleo ndani ya Halmashauri yetu ya Mtama.

Kwa niaba ya Wenyeviti  waliohudhuria kikao hicho, Ndg. Shabani Ally Jalasi ambaye ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Mihogoni Kata ya Mtama alitumia fursa hiyo kumpongeza Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha kwa ajili ya miradi hiyo huku akitoa wito kwa wajumbe kwenda kusimamia kikamilifu ili kuziunga mkono jitihada hizi za Serikali ya awamu ya sita. Aidha, alimshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtama kutokana na kutambua thamani na umuhimu wa Wenyeviti wa Vijiji huku akiahidi kuwa maelekezo yaliyotolewa  wameyapokea kwa lengo la kuyafanyia kazi. “ tunaenda kushirikisha jamii kwa kutumia vikao mbalimbali vya uhamasishaji ili wananchi wajitokeze kwa wingi kujitolea kwenye miradi hii ili ikamilike kwa wakati”.  Shabani Jalasi Mwenyekiti wa Kijiji cha Mihogoni.

Katika kuhitimisha maagizo yake Mkurugenzi aligawa vyeti vya Hati ya usajili wa Vijiji kwa Wenyeviti na kuwaeleza kuwa ataandaa ratiba ya kuendesha mikutano ya hadhara kwa wananchi katika vijii vyote vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama, ‘Mtama kwanza kwa Maendeleo’. 

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.