• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

MBUNGE ANAESHUGHULIKIA WAFANYAKAZI AFANYA ZIARA HALMASHAUURI YA WILAYA YA MTAMA.

Posted on: December 22nd, 2023

Mbunge wa viti maalaum anaeshughulikia wafanyakazi Mh. Dkt. Alice Karungi Kaijage amefanya ziara ya kutembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mtama kwa lengo la kusikiliza changamoto, ushauri na mapendekezo ya watumishi wilayani hapo.

Katika kikao kilichofanyika leo tarehe 22 Disemba, 2023 katika ukumbi wa Halmashauri, watumishi wa Halmashauri kwanza waliishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Raisi Daktari Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Mishaara kwa wakati, Kupunguza Kodi ya mshahara, kuripa madeni ya wafanyakazi lakini pia juhudi za Serikali kupandisha madaraja watumishi. Pili walitoa changamoto zao kama ifutavyo Serikali kuongeza mshahara, Serikali kupunguza kodi ya mshahara, Serikali kuwaendeleza watumishi kielimu, Serikali kutatua taharuki ya kikokotozi, changamoto ya utegemezi wa bima ya afya, kulipwa kwa wakati malipo ya likizo, kupandishwa madaraja, kubadili muundo wa upandishaji madaraja pamoja na ongezeko la fedha ya matumizi mengineyo (OC).

Mhe. Kaijage alipokea pongezi za watumishi kwa Serikali ya awamu ya sita na kujibu changamoto mbalimbali za watumishi na kuhaidi kuchukua changamoto hizo na kuzipeleka ngazi za juu. Aidha suala la kikokotozi Mhe. Kaijage alisema kuwa Raisi aliomba aachiwe suala hilo hivyo watumishi watulie kwa kuwa Raisi anafanyia kazi suala hilo.

Mhe. Kaijage aliongeza kuwa utegemezi wa bima ya afya ni changamoto iliyojirudia katika Halmashauri nyingi alizopita hivyo ataenda kuishauri idara ya afya kufanya ziara katika Halmashauri ili watoe elimu juu ya bima ya afya kwa wote, utegemezi wa bima ya afya lakini pia wasikilize changamoto na mapendekezo ya watumishi kuhusu bima ya afya.

Pamoja na hayo Mhe. Kaijage aliongeza kuwa ni jukumu lake kuhakikisha kuwa anatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), akisifu kuwa katika miaka miwili na miezi nane Serikali ya Awamu ya sita imeweza kupandisha madaraja watumishi 425,000 ambapo kwa mwaka inagharimu Serikali shilingi Tilioni 1.12 sambamba na hilo kwa upande wa ajira takribani watumishi 129,000 kutoka Serikali Kuu na 21,000 kutoka Serikali za Mitaa wameajiriwa.

Mhe. Kaijage aliongeza kuwa katika Sherehe za Meimosi zilizofanyika mwaka huu Raisi alisema kuwa taifa lolote linaloendelea chini yake kuna nguvu ya watumishi maneno hayo yanadhihilika katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo Serikali imeweza kuajiri watumishi 47,000 na kusema kuwa Serikali imeendelea kuwajali watumishi kwa kubadilisha miundombinu ya watumishi 3,345.

Alkadhalika Mhe. Kaijage aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mtama kwa kuwajali na kuwalipa watendaji wa kata na vijiji. Mhe. Kaijage alimaliza kwa kuishauri Halmashauri kuwa na utaratibu wa kufanya kikao mala kwa mala ili kutambua changamoto na kufanya suluhisho za changamoto hizo kwa wakati.

Afisa utumishi wa Halmashauri ndugu Kalingonji kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama ndugu Goerge Mbilinyi alimshukuru Mhe. Kaijage kwa ziara na hotuba yake mzuri kwa watumishi, ndugu Kalingonji aliongeza kuwa Halmashauri imepokea ushauri wa Mhe. Kaijage hivyo Halmashauri itaweka utaratibu sahihi wa vikao pia itaendelea kutatua changamoto za watumishi hasa watendaji wa kata na vijiji.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.