• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

MAAFISA MIFUGO NA UVUVI MTAMA DC WATATULIWA CHANGAMOTO YA USAFIRI

Posted on: February 1st, 2022

Kutokana na kuwepo kwa tatizo la usafiri,  changamoto inayosababisha Maafisa uvuvi na mifugo ngazi ya Kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama kushindwa kuwafikia wananchi, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetoa pikipiki mbili Wilayani humo kwa lengo la kuboresha huduma za ugani na kurahisisha namna ya kuwafikia wananchi.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa pikipiki hizo Afisa Mifugo Kata ya Sudi Bi. Jafarani Ally Mohammed, ameishukuru Serikali kupitia Wizara hiyo kwa kumaliza tatizo la usafiri hususani kwenye Kata yake huku akiongezea kuwa kutokana na uhaba wa usafiri, Idara ya Mifugo na Uvuvi ilishindwa kutekeleza majukumu kwa weredi  na kiwango cha juu, hivyo basi kupatikana kwa pikipiki hizo zitakwenda kurahisisha utendaji kazi kwa wakati na ufanisi kwa kuyafikia maeneo yasiyofikika kwa urahisi na kuweza kufanikiwa kudhibiti shughuli za uvuvi haramu lakini pia kutoa elimu pamoja na huduma mbalimbali kwa wafugaji.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Shaibu Ndemanga wakati akikabidhi pikipiki hizo alisema kuwa awali katika Halmashauri ya Mtama kulikua na tatizo la magonjwa kwa upande wa Mifugo na uvuvi haramu kwa sababu  Maafisa hao walikua wanashindwa kuwafikia wafugaji kwa wakati lakini pia kufanya doria za usiku ambapo amewataka kwenda kutekeleza majukumu yao kwa uzalendo wa hali ya juu.

Aidha Ndemanga alieleza kwamba kupatikana kwa pikipiki hizo zinakwenda kusaidia upatikanaji wa takwimu sahihi za mifugo, kutoa elimu za ufugaji bora kwa wafugaji pamoja na  kudhibiti utokeaji wa migogoro baina ya wakulima na wafugaji.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtama Ndg. George Mbilinyi ameishukuru Wizara ya Mifugo kwa kupeleka pikipiki hizo hali inayotajwa kwenda kuongeza mapato ya Halmashauri kupitia Idara ya Mifugo kwani wataalamu wataweza kuvifikia kwa haraka vyanzo vya mapato hususani wakati wa mauzo ya samaki.

Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekabidhi pikipiki 300 kwenye Halmashauri 184kwa awamu ya kwanza nchini ambapo Halmashauri ya Mtama imepokea pikipiki mbili zitakazohudumia Kata ya Sudi na Kiwalala.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.