• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE ATEMBELEA MIRADI SABA WILAYANI LINDI

Posted on: August 27th, 2021

Kiongozi wa mbio za Mwenge maalumu wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi , tarehe 27 Agosti 2021 ametembelea miradi 7 ya maendeleo Wilaya ya Lindi ambapo miradi 2 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama na miradi 5 Halmashauri ya Manispaa ya Lindi kwa lengo la kukagua na kuweka mawe ya msingi pamoja na kufanya uzinduzi katika miradi wa utoaji wa huduma za afya kwa mfumo wa Got-homis kwenye kituo cha afya cha Mnazi Mmoja.

Aidha miradi iliyotembelewa na mwenge huo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama ni pamoja na ujenzi wa barabara ya Mtama hadi mahakama ya mwanzo mita 800 kwa kiwango cha lami pamoja na mradi wa ujenzi wa maabara na matundu ya vyoo 6 katika shule ya sekondari Mtua.

Akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Mtama hadi mahakama ya mwanzo Mtama mkurugenzi wa TARURA Wilaya ya Lindi Eng. Dawson Paschal, amesema mradi huo ni miongoni mwa miradi mitano ya barabara inayotekelezwa na wakala wa barabara vijijini na mijini (TARURA) katika Halmashsuri ya Wilaya ya Lindi kwa mwaka wa fedha 2020/2021 ambao umegharimu kiasi cha Tsh. 296,690,000/= kwa awamu ya kwanza na tayari mkandarasi amelipwa kiasi cha Tsh. 271,550,000/= na kubaki kiasi cha Tsh. 25,140,000/= . Ameongeza kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022, mradi huo umetengewa kiasi cha Tsh. 80,150,000.00/=ambazo zitatumika katika utekelezaji kwa awamu ya pili. Aidha Eng. Dauson ameeleza kuwa, mradi huo ulianza tarehe 20 Januari 2021 na kukamilika tarehe 30 Agosti 2021 ambao umetekelezwa kwa awamu ya kwanza chini ya utekelezaji wa mkandarasi wa M/S SERC Constructin Ltd na kwamba mradi huu utapangiwa fedha kila mwaka ili kuweza kukamilika kwa usanifu wake.

Kukamilika kwa mradi huu kutasaidia watumiaji wa zahanati ya Mtama, Mahakama ya mwanzo lakini pia ni mpango na jitihada za kuboresha miji inayokua katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama.

Mradi mwingine ni ujenzi wa maabara ya sayansi na matundu sita ya vyoo katika shule ya sekondari Mtua ambao umetolewa taarifa za utekelezaji wake na mkuu wa shule hiyo Mwl.William Kanyondo na kusema mradi huo ulianza mwaka 2014 kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri pia ni miongoni mwa miradi 23 kupitia mpango wa Lipa kwa Matokeo ambao utagharimu kiasi cha Tsh 62,000,000/=hadi kukamilika kwake. Aidha ameeleza kuwa mradi huo umepokea Tsh 40,000,000/=za EP4R kutoka serikali kuu na Tsh 22,000,000.00/= kutoka Halmshauri ambapo kiasi cha Tsh. 15,000,000/= Za Halmashauri zimetumika katika ujenziwa vyumba viwili vya maabara na kiasi cha Tsh. 7,000.000/= zinatumika kwenye ujenzi wa matundu 6 ya vyoo vya wanafunzi na kwamba jumla ya Tsh. 56,075,639/= zimetumika na Tsh. 5,924,361/= zinzendelea kutumika katika shughuli za umaliziaji.

Sambamba na hilo kiongozi wa mbio maalumu za Mwenge wa Uhuru 2021 Luteni Josephine Mwambashi ametembelea miradi mitano katika Halmasahuri ya Manispaa ya Lindi ikiwemo mradi wa mfumo wa Got-homis katika kituo cha afya cha Mnazi Mmoja wenye gharama ya shilingi 34,524,500/=, mradi wa vyumba sita vya madarasa na matundu ya vyoo nane katika shule ya msingi Mnazi Mmoja uliogharimu shilingi 116,920,000/=, ametembelea mradi wa maji wa Tandangongoro wenye gharama za Tsh. 2,726,843,628.61/=, ametembelea mradi wa vikundi vya wajasiriamali vya wanawake, vijana na walemavu wenye jumla ya gharama ya Tsh 2,726,843,682.61/= lakini pia ametembelea mradi wa kituo cha mfumo wa taarifa za Kijiografia wenye thamani ya shilingi s123,529344/=

Aidha, wakati akitoa salamu na ujumbe wa Mwenge wa Uhuru 2021 kwa wananchi wa Wilaya ya Lindi, kiongozi wa mbio maalumu za Mwenge alieleza mambo muhimu ikiwemo matumizi ya malipo ya kielektroniki wakati wa ukusanyaji wa mapato kwa ngazi ya Halmashauri na kusisitiza zaidi kuhusu umuhimu wa risiti ya EFD. Lakini pia amewahasa wananchi juu ya matumizi sahihi ya TEHAMA huku akisisitiza zaidi kuwa na ushirikiano katika mapambano dhidi ya rushwa, malaria, UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya pamoja na ugonjwa wa COVID19 kwa la kuwa na taifa endelevu.

Katika Wilaya ya Lindi, jumla ya miradi 7 imetembelewa ambapo miradi 3 imezinduliwa, miradi 3 imewekwa mawe ya msingi na mradi mmoja umetembelewa. Mbio maalumu za Mwenge wa Uhuru 2021 zimehitimishwa tarehe 28 Agoti 2021 ukiambatana na kauli mbiu “TEHAMA NI MSINGI WA TAIFA ENDELEVU ITUMIE KWA USAHIHI NA UWAJIBIKAJI”.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.