• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

KATIBU MKUU JUMUIYA YA WAZAZI CCM TAIFA ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO MTAMA DC

Posted on: September 16th, 2021

Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa Ndg. Gilbert Kalima tarehe 16/09/2021 amekamilisha  ziara ya siku mbili katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama na kufanikiwa kutembelea na kukagua Miradi mbalimbali ya maendelea ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu aliambatana na uongozi wa Chama ngazi ya Taifa, Mkoa, Wilaya, pamoja na Mbunge wa Jimbo la Mtama Mh. Nape Nnauye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mtama Mh. Yusuph Abdallah Tipu na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ndg. George Emmanuel Mbilinyi.

Miongoni mwa Miradi aliyoitembelea ni pamoja na Mradi wa Hospitali ya Wilaya iliyopo Kata ya Kiwalala uliogharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.8,  Mradi wa umaliziaji wa maabara ya sayansi shule ya sekondari Mahiwa uliogharimu kiasi cha  shilingi 40,000,000/=, Mradi wa Maji wa Namupa unaofadhiliwa na Kanisa la Anglikan Dayosisi ya Masasi unaotumia zaidi ya shilingi  400,000,000/= pamoja na Mradi wa Barabara ya Mahakama ya Mwanzo Mtama uliotumia shilingi  296,690,000/= kwa hatua ya kwanza ya ujenzi wa barabara hiyo. Aidha Katibu Mkuu alipata nafasi ya kutembelea na kuzungumza na Wanachama wa CCM kupitia mashina yao ya Chama ili kuibua changamoto zinazowakabili ambapo alitembelea  Shina namba sita la Naijongolo Kata ya Nyangao pamoja na Shina namba nne la Msiondoke Kata ya Mtama ndani ya Jimbo la Mtama.

Akitolea ufafanuzi kwa changamoto zilizowasilishwa na Mkuu wa shule ya sekondari  Mahiwa Mwl. Onoratha Tarimo  kuhusu uhaba wa maji, ukosefu wa zahanati pamoja na usafiri; Mbunge wa Jimbo la Mtama Mh. Nape Mosses Nnauye amesema kuwa Serikali imetenga kiasi cha shilingi 75,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa zahanati itakayohudumia wanafunzi wa shule hiyo pamoja na jamii inayowazunguka, vilevile amewahakikishia wanafunzi hao  kupatikana kwa gari la shule ili kurahisisha usafiri wa wagonjwa. Aidha ametoa shukrani kwa Kanisa la Anglikan kwa kufadhili Mradi wa maji utakaowanufaisha wanafunzi wa shule hiyo pamoja na wananchi kwa ujumla.

Kadharika, Mh. Nape alitolea ufafanuzi kuhusu uhaba wa maji kutoka kwa wanachama wa Shina namba sita la Naijongolo Kata ya Nyangao  huku akisema  kuwa Serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 5 kwa ajili ya ukamilishaji wa mradi wa maji wa Chiuwe ili kusambaza huduma ya maji katika  Kata ya Nyangao pamoja na Makao Makuu ya Halmashauri.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa Ndg Gilbert Kalima alitoa pongezi kwa miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye Halmashauri hiyo lakini pia amewahakikishia wananchi kuwasilisha kwenye ngazi ya Taifa changamoto zilizotolewa katika maeneo aliyotembelea kwa utekelezaji zaidi. Ametoa wito kwa wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi kutoa hamasa na elimu kwa wananchi kwa lengo la kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022.


Ziara hii ya Sekreterieti ya Chama Chama Cha Mapinduzi Taifa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mama Samia Suluh Hassan kutembelea wanachama ngazi za mashina pamoja na matawi ili kuibua changamoto mbalimbali za wananchi na kuzifanyia kazi na kuweza kuimarisha Chama.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.