• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

HEART TO HEART FOUNDATION (HtHF) NA KAMPENI YA NYUMBA NI CHOO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA.

Posted on: December 18th, 2023

Vijiji kumi vya Kata ya Nyangao na Namangale vimeendesha uhakiki binafsi wa hali ya uboreshaji wa vyoo katika kaya. Vijiji hivyo vimetekeleza kazi hiyo kwa uwezeshwaji wa Shirika lisilokuwa la serikali la Heart to Heart Foundation linalofanya kazi na Halmashauri ya Wilaya ya Mtama, Shirika hilo linaunga mkono kampeni ya Nyumba ni Choo katika kata mbili, kata ya Nyangao na kata ya Namangale ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mtama. Tangu mwezi Machi 2023 shirika la HtHF limejikita katika kata hizo mbili kutekeleza afua ya Kampeni ya usafi wa mazingira ili kupambana na kupunguza magonjwa ya kuambukiza yatokanayo na uchafu wa choo kama vile kuhara, kuhara damu, homa ya matumbo na kipindupindu.

Heart to Heart Foundation limesaidia sana jamii ya kata hizo kujua mapungufu waliyokuwa nayo na hivyo kupitia elimu juu ya umuhimu wa choo bora iliyosisitizwa, wananchi sasa wanaelewa choo bora lazima ijengwe kwa kuzingatia sifa tano muhimu ambazo ni sakafu inayosafishika, jengo imara lililojengwa kwa miti na udogo au tofali, mlango unaofungika na unaotunza siri, paa lililoezekwa vizuri na kuzuia mvua isiharibu shimo la choo na mfuniko usiopitisha harafu na wadudu kama vile inzi na mende.

Katika zoezi hilo Afisa Afya wa Halmashauri Bwana Elvan Limwagu akiwa na timu yake,  wakishirikiana na Mratibu wa Shirika la HtHF Bwana Eston Waliha walifanya ufuatilia wa mikutano ya uhamasishaji iliyofanyika ngazi ya vitongoji kwa lengo la kusisitiza kaya zote ndani ya vijiji vya kata hizo ziwe na vyoo bora kabla ya uhakiki. Aidha Afisa Afya wa Halmashauri alitoa pongezi kwa viongozi wa kata, vijiji na vitongoji kwa ushirikiano wao na wananchi na kuwezesha kufikia asilimia 70 ya kaya zote kuwa na vyoo bora ndani ya kipindi cha utekelezaji huo. Afisa Afya Limwagu amewataka viongozi hao kuongeza bidii, juhudi na hamasa kufikia lengo la mradi huo ifikapo Febuari 2024.

Aidha Mratibu wa Heart to Heart Foundation ndugu Eston Waliha amebainisha kuwa Mafanikio ya mradi huo katika vijiji vya kata hizo utawezesha kazi za mradi huo kupanuliwa na kuzifikia kata zingine zaidi hapo mwakani lengo likiwa ifikapo mwaka 2026 kaya zote katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama viwe na vyoo bora na kuwezesha upatikanaji wa maji safi na salama katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kuongeza na kuimarisha utoaji wa huduma za afya zilizo bora.

Sambamba na ilo Ndugu Limwagu aliongeza kuwa mradi huo umefanikiwa kwa

kupunguza magonjwa yanayozuilika kwa matumizi sahihi ya choo na unawaji wa mikono baada ya kutoka chooni na hivyo idadi ya wagonjwa wanaohudhuria hospitali kupungua. Aliwataka wananchi wote kutopuuza elimu wanayopata na kwamba waendelee kuhamasishana kujenga vyoo bora ili kutimiza lengo la mradi huu, pia HtHF limesaidia kujenga vyoo vinne vya mfano (choo moja kwa kila kijiji) katika kijiji cha Mahiwa, Namangale, Mawilo na Mtakuja II kwa kaya nne zisizojiweza ili wananchi waone na kuiga. #USICHUKULIE POA NYUMBA NI CHOO.



Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.