• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

DED MTAMA AWAPONGEZA WANANCHI WA MTUALONGA

Posted on: November 3rd, 2021

Pongezi hizo zimetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama Ndg. George Emmanuel Mbilinyi kufuatia Mpango mkakati wa wananchi wa Kijiji cha Mtualonga kukubaliana  kuchangia fedha shilingi 3,000/= na matofali 2 ya nchi 6 yenye kiwango na ubora sawa ili kuendeleza ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kata itakayojengwa kwenye kijiji cha Tulieni kwa lengo la kupunguza hadha ya usafiri inayowakumba watoto wao wakati wanapohitaji kwenda shuleni. 

Mkurugenzi alikutana na wananchi wa kijiji hicho kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika tarehe 2/11/2021  na kutoa maelekezo ya utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa kituo shikizi chenye vyumba 2 vya madarasa kijiji cha Nammeda. Katika mkutano huo Mkurugenzi aliambatana na timu ya Wataalamu wa Halmashauri (CMT) kutoka idara mbalimbali ambao walipata nafasi ya kujibu na kutolea ufafanuzi wa hoja na changamoto zilizotolewa na  wananchi hao.

Kabla ya kusikiliza hoja, maoni na changamoto Mkurugenzi aliwataka viongozi kwa ngazi ya Kijiji na Kata kuhakikisha Mradi huo unasimamiwa kwa umakini, uzalendo na ushirikiano na wanajamii.  Aidha amesisitiza kutumia rasilimali zilizopo ili kupunguza gharama za ujenzi. Sambamba na hilo, Mkurugenzi huyo aliwaomba wazee wa kijiji hicho kuunda baraza la wazee litakalojikita katika kutoa ushauri, kukosoa pamoja na kurekebisha makosa yanayofanywa na viongozi mbalimbali. Aliwaeleza kuwa wazee wa kijiji wana   nafasi ya kukutana na kutoa mawazo na ushauri pindi wanapoona kuna dosari katika utekelezaji wa majukumu yao. Aidha, wazee hao wamemuhakikishia kuwa kupitia baraza watakaloliunda watafanya tathimini ya maendeleo ya miradi mbalimbali kila baada ya miezi 3 ili kuchochea suala la uwajibikaji katika shughuli mbalimbali kwenye jamii.

Katika kikao hicho, wananchi walieleza kero zao ikiwa ni pamoja na licha ya kukatwa fedha kwa ajili ya bima ya afya iliyoboreshwa (ICHF) lakini bado hawajapata huduma hiyo pia walihoji kuhusu mikopo ya vikundi kutotolewa kwa wakati.

Akitolea ufafanuzi wa hoja ya bima ya afya iliyoboreshwa, Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Dismas Masulubu amesema kuwa kutokana na changamoto ya urekebishaji wa kadi za awali ilipelekea kuchelewa kwa zoezi la uandikishaji lakini kwa sasa kadi hizo tayari zimeshapatikana na   timu ya wasajili inaendelea na kazi hiyo hivyo basi kwa mwanchi  yeyote ambaye hajapata huduma hiyo anatakiwa kujitokeza kujisajili siku ya tarehe 6/11/2021 wakiwa wamekamilisha kaya zao huku akifafanua kuwa bima hizo zitafanya kazi  kwa mwaka mzima kuanzia siku ya kujiandikisha na kwamba bima hizo zinatumika kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya vya serikali pekee.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Bi. Sharifa Tapalu alitolea ufafanuzi wa upatikanaji wa mikopo ambapo alisema kuwa mikopo hiyo inatolewa kwa vikundi vya vijana  wenye umri kuanzia miaka 18-33, wanawake pamoja na watu wenye ulemavu hivyo basi ili vikundi hivyo viweze kupata mikopo ni lazima  viwe na shughuli maalumu ya kijasiliamali  ili  fedha hizo ziendeleze miradi hiyo. Aidha alisistiza umuhimu wa kulipa fedha za mikopo  ya awali ili kuisaidia Halmashauri kuendelea kutoa fedha kwa vikundi vingine.

Naye Muweka Hazina wa Halmashauri CPA Asha Msangi alitumia fursa hiyo kusisitiza juu ya suala la ukusanyaji wa mapato  kwa kuendelea kulipa ushuru lakini pia amewataka wananchi hao kila mmoja awe mlinzi kwa mwenzake katika kusimamia na kumsaidia  Mtendaji wa Kijiji katika kufuatilia watu wasiolipaa ushuru wa shughuli zao za kiuchumi.

Mtendaji wa Kata ya Longa Bw. Oscar Daudi Millanzi alitoa shukurani kwa Mkurugenzi kwa kupeleka nguzo za umeme kwenye Mradi wa maji wa Mtualonga na kwamba kwa sasa huduma ya maji inapatikana katika kijiji hicho.

Wananchi wakiwa kwenye mkutano

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.