• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

DED MTAMA AGAWA VIFAA VYA MICHEZO

Posted on: August 25th, 2021

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama George Mbilinyi leo tarehe 25 Agosti 2021 ametoa vifaa mbalimbali vya michezo  ikiwemo mipira ya miguu kwa timu  ya mpira wa miguu ya Mtama Boy's kwa lengo la kuunga mkono jitihada zinazofanywa na vijana hao katika kuendeleza  michezo katika Halmashauri hiyo. Hafla ya kukabidhi vifaa hivyo imefanyika katika maeneo ya Halmashauri na kuhudhuriwa na  Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mh. Othmani Ongonyoko, Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Yusufu Tipu, Afisa michezo Masoud Elewa pamoja na mdau wa michezo Selemani Mathew. 

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Mbilinyi amewataka vijana hao kuwa na tabia ya kufanya mazoezi mara kwa mara kwani yatawasaidia kufanya vizuri katika mpira wa miguu, na kusisitiza kuwa mazoezi ni afya, michezo ni burudani lakini pia ni fursa ya ajira. Aidha Mbilinyi ameahidi kuwa Halmashauri yake itaendelea kulipa kipaumbele suala la michezo na kuendelea kutoa mchango katika sekta hiyo kwani kuna vijana wengi wana vipaji vya kucheza mpira wa miguu hata hivyo hawajapata fursa ya kuonekana kutokana na changamoto ya vifaa  jambo ambalo linasabisha kushindwa kuonesha vipaji vyao. “tumepata mipira hii saba pamoja na vifaa vingine vya kuanzia  lakini tunatarajia ndani ya wiki hii tutakamilisha vifaa vilivyopungua. Lengo letu ni  kutengeneza timu imara ya Mtama ambayo ni Mtama Boys itakayounda timu ya wachezaji ambao wataenda kusaidia timu ya Namungo ili tuweze kupunguza makali ya kusajili wachezaji kutoka nje ya nchi. Michezo ni "platform" na kiungo muhimu  kati ya serikali , Chama pamoja na wananchi hata Mwalimu Nyerere alitumia sekta ya michezo katika harakati za kudai uhuru lakini pia michezo ni sehemu nzuri ya kufikisha ujumbe kwa jamii hivyo tujikite zaidi katika sekta hiyo.  .Sasa hivi mpira unalipa sana  umesaidia vijana wengi wa Kitanzania kunufaika Kutokana na michezo ,hivyo natumaini mipira hii inakwenda kusaidia kuibua vipaji vya vijana katika halmashauri hii na kuweka kupata timu itakayoshiriki ligi daraja la kwanza ikiwezekana ligi kuu.” amesema Mbilinyi. Pia Mh. Mbilinyi ameahidi kuibua vipaji na michezo mingine ikiwemo mchezo wa bao ndani ya Halmashauri ya Mtama.

Kwa upande wake mdau wa michezo Selemani Mathew  amempongeza Mkurugenzi huyo kwa kutoa vifaa huku akitoa wito kwa wadau wengine wapenda michezo kujitokeza kuwaunga mkono kwani bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo Jezi,viatu nakadhalika.

Akitoa shukurani mara baada ya kupokea vifaa hivyo Nahodha wa timu hiyo Twaha Kabongo amemshukuru Mkurugenzi na kuahidi kuwa atahakikisha kuwa vifaa hivyo watavitunza na kuvitumia ipasavyo kwa lengo lililokusudiwa na kuongeza kuwa hawatomuangusha kwani dhamira yao ni kuona vijana wengi miongoni mwao wanapata nafasi ya kuchezea Ligi Kuu Tanzania Bara na hata nje ya Nchi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.