• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

DED AKERWA NA HALI YA STENDI MTAMA

Posted on: October 29th, 2021

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama Ndg. George Emmanuel Mbilinyi amekiri kutoridhishwa na hali iliyopo kwenye kituo cha mabasi Mtama kutokana na kukosa vigezo na hadhi kwani kituo hicho kwa sasa hakina  sehemu za chakula wala maeneo ya  kupumzika abiria.

Amezungumza hayo jana tarehe 29/10/2021 kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Robo ya Kwanza 2021/2022 uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri wakati akitolea ufafanuzi wa hoja iliyotolewa na diwani wa Kata ya Mnara Mh. Athumani Mpole kuhusu hali ya kituo hicho. Amesema kuwa licha ya stendi hiyo kukusanya mapato ya Tsh. 10,000,000/= kwa mwezi  lakini bado huduma zinazopatikana haziridhishi hivyo ametuma wataalamu wake wa Halmashauri kwenda kujifunza kwenye stendi ya Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara ili wafanye maboresho ya kituo hicho.

Mkurugenzi amesema kuwa Kuhusu suala la ushirikishwaji wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo ambalo limekuwa likilalamikiwa na Madiwani wengi kwenye Baraza hilo, Mbilinyi ataahakikisha kuwa kuanzia sasa madiwani hao watashirikishwa kila hatua ya miradi kupitia vikao mbalimbali lakini pia atafanya ushirikishwaji kwa wananchi pamoja na viongozi wa Vijiji na Kata.

" tukitaka  tuirekebishe na kuijenga Mtama ni lazima tufikirie kuwa sisi ni Watanzania na ni  lazima tuwe na ushirikiano baina ya Madiwani na Watumishi wa Halmashauri" Tusipokuwa na umoja na kukosa  ushirikiano hatutaweza kufikia malengo yetu. Mimi nikiwa kama kiungo muhimu naahidi kwamba naenda kuwaunganisha na kuwa kitu kimoja." George Mbilinyi Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya  Mtama.

Sambamba na hilo, Ndg. Mbilinyi amesisitiza matumizi ya rasilimali zilizopo kwenye maeneo ambayo miradi inaendelea hususani Miradi ya ujenzi wa madarasa kupitia fedha za UVIKO19 ili kupunguza gharama na kuepuka ubadhirifu wa fedha huku akiongeza kuwa kwa kufanya ivo kutatoa fursa kwa wananchi kujipatia kipato kupitia shughuli za uuzaji wa malighafi ya ujenzi kama vile kokoto na mchanga.

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Lindi Ndg. Thomas Safari amewataka Madiwani pamoja na wataalamu wa Halmashauri kufanya kazi kwa umakini na umoja ili kukamilisha Miradi iliyopokelewa lakini pia kuhakikisha thamani ya fedha iliyotumika inaendana na viwango vya jengo husika.

Wajumbe wa Baraza hilo wamempongeza Mkurugenzi kwa kuonesha njia bora ya mafanikio na kuhahidi kuwa watamuunga mkono katika kila hatua ya maendeleo kwa lengo la  kuleta mabadiliko ndani ya Halmashauri. "Baraza la leo tumelipokea vizuri na tuna matumaini kwa kiongozi wetu kwani asilimia kubwa ya jitihada zake zinaendana na matamanio yetu, kwaiyo nitoe wito kwa madiwani wenzangu tukasimamie majukumu katika maeneo yetu ya kazi na tuondoe matabaka kati ya watumishi na Madiwani hii itasaidia kuiendeleza  Mtama yetu". Hamza  Nguwachi Diwani Kata ya Nahukahuka.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • RAS LINDI AIPONGEZA HALMASHAURI YA MTAMA KWA KUPATA HATI SAFI

    June 18, 2025
  • DKT CHILUMBA AWAASA WAUGUZIBKUZINGATIA MAADILI YAO YA KAZI

    June 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.