• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

NDEMANGA AIPONGEZA KAMATI YA LISHE MTAMA DC

Posted on: December 7th, 2021

Mkuu wa wilaya ya Lindi Mhe. Shaibu Ndemanga, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mtama kwa kufanya jitihada kubwa ya kuzingatia suala la lishe kwa kufanya vikao  vya mara kwa mara kulingana na mujibu wa Kalenda pamoja na jitihada wanayozozifanya katika kuwasilisha taarifa Mkoani.

Ndemanga ameyasema hayo tarehe 06/12/2021 aliposhiriki katika kikao cha Kamati ya Lishe na kuongeza kuwa  zipo baadhi ya Halmashauri ambazo zinafanya vikao hivyo mara chache na wengine kutofanya kabisa, jambo linalosababisha changamoto katika ngazi ya mkoa kwa kutojua nguvu ziwekezwe vipi katika Halmashauri ili tatizo la lishe liweze kumalizika.

Aidha, Licha ya vikao kufanyika mara kwa mara, bado Halmashauri ya Mtama na Mkoa wa Lindi kwa ujumla unaonekana upo nyuma kwenye maendeleo ya Lishe. Na hii ni kwa sababu ya Nyanja zingine tofauti na vikao kusuasua. Ndemanga amemuagiza Mkurugenzi na watendaji wengine, kufuatilia vigezo vingine vya lishe kama zoezi la mtoto kuchangia shilingi elfu moja na kujihusisha na shughuli au miradi inayohusiana na suala la lishe ili baadae waweze kutambua ni lipi halijafanyika na kuweka mazingira ya kulifanya.

Suala la lishe limekuwa likiendana moja kwa moja na changamoto ya Utapiamlo. Lindi ni kati ya Mikoa iliyo na tatizo hilo jambo ambalo limekuwa likiwashangaza wengi kwakuwa vyakula bora vyote vinapatikana kwa gharama nafuu na baadhi vimekuwa vikipatikana bure. Hivyo Ndemanga ameitaka Halmashauri ya Mtama kutathmini ni wapi kuna changamoto hii kwa ukubwa ili waweze kutoa elimu zaidi kwa wananchi wake kwa sababu vyakula vipo, lakini changamoto ni jinsi gani wanavitumia vyakula hivyo kuondokana na tatizo la utapiamlo.

Aidha, ameipongeza Halmashauri katika suala la ujenzi wa madarasa ya COVID 19 na kukiri kuwa Halmashauri hiyo  ililegalega hapo awali, lakini kutokana na jitihada za usimamizi zinazofanywa hadi kufikia tarehe 15 mwezi Disemba  Mtama inaweza kushika nafasi ya kwanza katika Halmashauri zinazofanya vizuri kwenye ujenzi wa madarasa hayo. “Tunaweza tusimalize madarasa yote kwa asilimia mia moja, lakini na sisi tutakuwa na madarasa yaliyokamilika, lakini hatutokuwa na darasa lililo katika msingi…” Ndemanga.

Licha ya miradi hiyo kuhitaji jitihada kubwa ya usimamizi kwa sasa kutoka Halmashauri, bado amewataka viongozi kutoisahau miradi mingine ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani humo.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.