• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

DC NDEMANGA AKUTANA NA WANANCHI WA MBUTA NA LITIPU WILAYANI MTAMA

Posted on: August 24th, 2021


Mkuu wa Wilaya Lindi, Mh.Shaibu Ndemanga, amefanya mkutano kwa nyakati tofauti  katika kijiji cha Mbuta, kata ya Mnolela pamoja na Litipu, kata ya Nyangamara katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama. Mkutano huo ulikuwa na lengo la kutambulisha Mradi wa uwekezaji wa Shamba la Pamoja na Kiwanda cha Miwa kutoka kampuni ya “SJ Sugar Company”  inayomilikiwa na Muhindi. Aidha, mikutano hiyo ililenga kutatua migogoro iliyojitokeza hapo awali, kati ya watumiaji wa eneo la mradi huo kutoka katika vijiji jirani vya Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, mkoani Mtwara.

Akitolea ufafanuzi juu ya umiliki wa eneo hilo, Mh.Shaibu Ndemanga, amesema kuwa, Mmiliki rasmi wa eneo hilo ni  Serikali na kwamba kabla ya Wananchi kujishughulisha na shughuli za kilimo katika Shamba hilo, eneo lilitengwa kwa ajili ya Malisho ya Mifugo. Aidha, mkuu wa Wilaya ameongezea kuwa  katika umiliki wa  eneo la Mradi huo jumla  ya hekari 2059.7, kati ya hekari zaidi ya 8000 ya Shamba zima ni mali ya Wilaya ya Lindi.

Pia amesema kuwa kulingana na hali ya umiliki kuwa ni ya Mikoa Miwili, Serikali imemtaka Mwekezaji huyo kabla ya kuanza rasmi shughuli za uwekezaji , kutoa “ Kifuta Jasho” kwa Watumiaji wa eneo hilo. Sambamba na hilo, Mkuu wa Wilaya amewaelekeza Wataalamu wa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama,  kuanza zoezi la Utambuzi wa Watumiaji haraka iwezekanavyo ili wananchi hao wapate stahiki zao. Katika Makubaliano kati ya Mmiliki na Mwekezaji, Serikali imemtaka Mwekezaji huyo kutoa mafunzo ya Kilimo cha Miwa, kutoa Mbegu bora za Miwa pamoja na kufungua fursa za soko kwa wakulima wadogo.

Shamba hilo lipo katika mpaka wa Mkoa wa Mtwara  na Lindi na lina ukubwa wa zaidi ya hekari  8000 ambapo  kati ya hekari hizo jumla ya hekari 2059.7 lipo katika Wilaya ya Lindi na hekari zilizobakia  zipo katika Wilaya ya Mtwara vijijini. Vijiji vilivogusa shamba hilo ni pamoja na Litipu na Mbuta katika Wilala ya Lindi, na kijiji cha Lilido kwa upande wa Mtwara

Hapo awali, Mkuu wa Wilaya, alipata fursa ya kuwapongeza Wananchi wa Kijiji cha Mbuta, kwa kuwa na moyo wa kujitolea kurekebisha barabara ya Mnolela-Mbuta na kuwahakikishia kilio cha barabara kimefika tamati kwani  Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 600 kwa ajili ya utengenezaji wa barabara hiyo kwa kiwango cha Kifusi na Changalawe. Mh. Ndemanga, amewaeleza  Wananchi wa Mbuta na Litipu kuwa Serikali imejipanga kusogeza huduma za Afya, umeme pamoja na maji na kwamba tayari Wakala  wa Umeme Vijijini (REA) kupitia Mpango wa Usambazaji wa Umeme ndani ya miezi 18, wapo katika hatua za awali za utekelezaji.

Vilevile, ametoa wito kwa Vijana na Wananchi wa Mbuta na Litipu, kuwa na utayari wa kutumia Umeme huo kwa shughuli za Maendeleo, pamoja na kujikita zaidi kwenye kilimo cha miwa na kuchangamkia fursa katika Mradi huo wa Uwekezaji na amewasisitiza zaidi wananchi hao kuacha tamaduni za kuuza maeneo yao kiholela.

Kwa upande wa Mmoja wa wakazi wa Mbuta Bw. Mohamedi Hamisi Mkulula , alitoa shukurani kwa niaba ya Wananchi kwa ujio na ripoti iliyowasilishwa na Mkuu wa Mkoa, huku akiahidi kuwa wako tayari kujitolea zaidi katika ujenzi wa Zahanati ya Mbuta, kwani, tayari Kijiji kimetenga eneo na wapo katika hatua ya kutoa Michango kwa hiyari.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA LISHE YAFANYA KIKAO CHA TATHMINIYA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE KWA ROBO YA TATU HALMASHAURI YA MTAMA

    June 04, 2025
  • MIRADI 7 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 2.7 YAPITIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MTAMA

    May 27, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.