• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Mali Asili
      • Afya
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Nyuki
      • Ununuzi na ugavi
  • Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • PICHA
    • MATUKIO
    • HOTUBA
    • HABARI
  • Mifumo
    • ffars
    • National Sanitation Compaign
      • E-learning
    • Sensa Elimu Msingi
    • Wajasiliamali
    • Government mail System
    • Madeni-Demo

BODI YA AFYA YAZINDULIWA MTAMA DC.

Posted on: November 2nd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Lindi Ndg. Shaibu Ndemanga  leo tarehe 2/11/2021 amezindua rasmi Bodi ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Mtama itakayoshughulika na kusimamia huduma zinazotolewa kwenye vituo mbalimbali vya Afya. Uzinduzi huo umefanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  na kuhudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Geoge Emmanuel Mbilinyi pamoja na baadhi ya Wataalamu wa Halmashauri hiyo. Tukio hilo lilihusisha pia uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo.

Kabla ya uzinduzi huo, Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Dismas Masulubu aliwaeleza wajumbe wa bodi hiyo  baadhi ya majukumu yao ikiwa ni kuhakikisha wanasimamia utoaji huduma katika ngazi za zahanati, vituo vya afya na hospitali, kusimamia upatikanaji wa watumishi, miundombinu pamoja na vitendea kazi.  Aidha Dkt. Dismas alitoa rai kwa wajumbe wa Bodi kuhakikisha wanaenda kupunguza vifo vya mama na mtoto lakini pia kuwa mabalozi katika uhamasishaji kwa wananchi ili waweze kupata chanjo ya UVIKO19 na chanjo za kawaida.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Lindi ambaye pia aliwataka wajumbe wa bodi hiyo kukutana vikao vyote vya kisheria bila kujali maslahi yao binafsi,  kufahamu na kufanyia kazi changamoto mbalimbali zinazojitokeza, kujua dawa zinazopelekwa kwenye vituo vya kutolea huduma kama zinatolewa ipasavyo kwa walengwa, kuwa na mahusiano mazuri na taasisi binafsi zinazotoa huduma za afya, kujua mipaka ya kikazi kati ya bodi, kuchuja mambo muhimu ya kupeleka katika ngazi ya halmashauri pamoja na  kupitia mirejesho inayopitishwa na halmashauri tayari kwa utekelezaji. Aidha, alitoa rai kwa wajumbe wa bodi hiyo kutojihusisha na siasa katika utekelezaji wa majukumu yao na badala yake wanatakiwa kusikiliza maoni ya viongozi au watu mbalimbali bila kujali itikadi zao za chama ili kuleta ufanisi katika uwajibikaji.

Nae mwenyekiti wa Bodi hiyo ambae alichaguliwa Ndg. Mohamedi Chilumba alitoa neno la shukurani kwa kuaminiwa kuwa kiongozi lakini pia alimuhakikishia Mkuu wa Wilaya kuwa Bodi ya awamu hii ni ya kipekee na kwamba inakwenda kusimamia na kutekeleza majukumu yao kwa kushirikiana na wataalamu wa Idara ya Afya na wananchi kwa ujumla.

Bodi ya Afya ya Halmashauri na Kamati za Afyaza Vituo vya kutolea huduma zipo kwa mujibu wa sheria ndani ya Hati Rasmi chini ya Sheria Sura Na. 287 na 288 ya Sheria ya mwaka 1993. Kufuatia sheria hiyo, wajumbe wa bodi waliochaguliwa kutoka katika vijiji vyao walifanya uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu ambapo Ndg. Mohamedi Chilumba alipita bila kupingwa huku Bi. Moza akichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti. Bodi hiyo itakuwa madarakani kwa muda wa miaka 3 na itafanya  kazi kwenye zahanati 28, vituo vya afya 4, pamoja na hospitali 2.

Mwenyekiti wa baodi Bw. Mohamedi Chilumba akitoa neno la shukurani baada ya kuchaguliwa

wajumbe wa bodi wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Ndg. Shaibu Ndemanga na baadhi ya Wataalamu wa Halmashauri


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWQENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA MIPAKA YA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MTAMA. September 16, 2024
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA ZOTE September 09, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA WATENDAJI MTAMA DC September 09, 2023
  • Angalia yote

Habari mpya

  • KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MTAMA

    May 09, 2025
  • DC MWANZIVA AMEITAKA KAMATI YA AFYA HALMASHAURI YA MTAMA KUONGEZA UHAMASISHAJI KWA WANAUME KUHUSU UMUHIMU WA LISHE

    April 29, 2025
  • DC MWANZIVA ASISITIZA KUDUMISHA MUUNGANO LINDI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI YATOA ELIMU KUHUSU NYONGEZA YA DOZI YA CHANJO YA POLIO HALMASHAURI YA MTAMA

    April 24, 2025
  • Angalia yote

Video

Risala ya utii kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Youtube
  • Mfumo wa Elimu Msingi na Sekondari
  • FOMU YA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA
  • Watumishi Portal

Tovuti Mashuhuri

  • Presidential office and Regional Secretariety
  • Electronic Goverment Agent
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Raisi-UTUMISHI
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Box 328 Lindi

    Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc

    Simu ya mezani: 0222061

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@lindidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya ndani
    • Katazo
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.