Mgeni Rasmi wa maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani DKT:Chilumba kutoka Ofisi ya Mganga mkuu Mkoa wa Lindi kwa niaba ya RMO Mkoa amewaasa wauguzi kuhakikisha wanazingatia maadili ya kazi yao ikiwa ni pamoja na kuzingatia matumizi ya lugha nzuri kwa wagonjwa, Maadhimisho hayo yamefanyika kimkoa leo tarehe 13 juni 2025 katika viwanja vya sokoni vilivyopo kata ya Majengo Halmashauri ya Wilaya ya Mtama.
“Wauguzi mnatakiwa kuhakikisha mnatoa huduma za afya zinazozingatia ubora wa kazi zenu ikiwa ni pamoja na kuzingatia utu, stara na lugha njema kwa wagonjwa lakini pia mnapaswa kuzingatia miongozo mbalimbali ya Serikali na taaluma yenu ili kuweza kukidhi ubora wa huduma mnazozitoa’’ alisema DKT:Chilumba.
Aidha wauguzi kutoka Mkoa wa Lindi wameahidi kuwa wataendelea kuzingatia miiko na maadili ya kazi yao lakini pia kufanya kazi kwa weledi ili kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania DKT:Samia Suluhu Hassani katika harakati zote anazozifanya za kuhakikisha sekta ya Afya inakuwa bora kwa kimbilio la Wanaanchi.
Lakini pia Maadhimisho hayo yaliambatana na maandamano ya Amani kutoka kituo cha afya Mtama hadi viwanja vya sokoni vilivyopo kata ya majengo lakini pia wauguzi walifanya matendo ya huruma kwa kutoa mahitaji mbalimbali kama vile sabuni kwa wagonjwa waliopo katika wodi ya watoto na watu wazima ndani ya kituo cha afya Mtama.
Box 328 Lindi
Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc
Simu ya mezani: 0222061
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@lindidc.go.tz
Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.