UTANGULIZI
Idara ya usafi na mazingira ni idara iliyoanzishwa kwa lengo la kusimamia na kuratibu maswala yote yanayohusu usafi na mazingira nchini. Malengo ya idara ni kusimamia uboreshaji wa usafi wa mazingira na Mazingira katika nchi na hatimaye kupunguza kama siyo kuondoa kabisa magonjwa na madhara yote ya kiuchumi. Kijamii na kisiasa yanasababishwa na uchafuzi na uharibifu wa mazingira. Hii inatokana na tafiti kwamba nchi zinazoendelea zinasadikiwa kutumia 5% ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kuhudumia madhara yatokanayo na uchafuzi wa mazingira kila mwaka (UNICEF) pia kupitia tafiti inakariwa kuwa kwa mwaka mmoja ulimwenguni vinatokea vifo 1.4 milioni vya watoto vinavyoweza kuzuilika. Vifo hivi vinasababishwa na madhara ya uchafuzi wa mazingira, hii ni sawa na watoto 4,000 kila siku kwa wastani wa mtoto mmoja (1) kila baada ya sekunde 20.
MAJUKUMU YA IDARA YA USAFI NA MAZINGIRA
|
Kuandaa na Kusimamia utekelezaji wa Sera ya Mazingira ya mwaka 1997; Kusimamia utekelezaji wa sheria ya mazingira Na 20 ya 2004; |
|
Kutoa ushauri kwa kamati ya mazingira ya wilaya katika masuala yanayohusu usimamizi na uendelezaji wa mazingira katika wilaya
|
|
Kufanya uraghibishi wa elimu ya mazingira
|
|
Kukusanya na kutunza taarifa za mazingira na matumizi ya rasilimali asilia
|
|
Kuandaa, kufuatilia, kufanya mapitio na usahili wa tathmini ya athari za mazingira (approval of the environmental impact assessment).
|
|
Kupitia na kuzifanyia marekebisho sheria ndogo za usimamizi wa mazingira za vijiji na halmashauri ya wilaya (by laws), na kazi za idara katika halmashauri ya wilaya zinazohusiana na mazingira
|
|
Kutoa ripoti kwa Mkurugenzi Mkuu na Mkurugenzi Kiongozi wa Mazingira, Kuratibu maadhimisho ya siku ya mazingira duniani
|
|
Kufanya tathmini ya athari ya mazingira katika miradi na kuhakiki tathmini ya athari kwa mazingira
|
|
Kudhibiti uharibifu na kuhifadhi mazingira ya asili, Kusimamia utawala kwa watumishi idara ya Usafi na Mazingira
|
|
Kufanya ukaguzi wa Afya ya Jamii (Public health Inspect)
|
|
Kufanya uhakiki na kupitisha mipango ,michoro na ramani ya ujenzi (Scrunitiny and approval of building plan)
|
|
Kusimamia udhibiti wa taka ngumu na taka kimiminika (Waste management)
|
|
Kusimamia usalama wa afya mahali pa makazi ( Occupational health and safety)
|
|
Kukuza na kuendeleza afya na usafi (Health promotion), Kukagua usalama, ubora na usafi wa chakula (Food safety and hygiene)
|
|
Kudhibiti magonjwa yanayoambukizwa na yasiyo ambukizwa (Communicable diseases and non communicable diseases control
|
|
Kudhibiti uchafuzi wa Mazingira (Pollution control), Kusimamia na kudhibiti wa majanga (Disaster Management)
|
|
Kufanya Chanjo (Vaccination), Kusimamia Afya na usafi mjini na vijijini (Hygiene and sanitation)
|
|
Kudhibiti wadudu hatari kwa binadamu na mazingira wanaoruka na wanaotambaa (Vector and venin control)
|
|
Kuzika miili iliyokufa (Disposal of the dead), Kudhibiti magonjwa ya milipuko (Diseases surveillance and response)
|
|
Kufanya mafunzo juu ya sayansi ya afya ya mazingira (Conduct training related to environmental health sciences)
|
|
Kuzuia na kudhibiti ajali (Accidental prevention and control), Kudhibiti usalama na ubora wa Maji (Water safety and quality control)
|
|
Kufanya tathimini ya athari ya afya ya mazingira (Carrying out environmental healthy impact assessment)
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Box 328 Lindi
Sanduku la Barua: 328 Lindi Dc
Simu ya mezani: 0222061
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@lindidc.go.tz
Copyright ©2021 Mtama District Council All rights reserved.